|
Gaetano Catanoso
(1879-1963)
foto
Myaka ya majifunzo
GAETANO CATANOSO alizaliwa pa « Chorio wa mtakatifu Lorenzo », katika
arkidioseze ya « Reggio Calabria », tarehe 14/02/1879. Baba yake Antonio
Katanoso na mama yake Antonina Tripodi walikuwa walimaji na wakristu wenyi
kukamilika. Siku hiyo yenyi alizaliwa, amepata pia Sakramenta ya Ubatizo; na kwa
mwaka 1882 alipata Sakramenta ya Uzabitisho.
Alipokuwa na umri wa myaka kumi, akasikia ndani mwake Uwito wa kuwa Padri. Ndipo
akaingia kwa Seminario ya « Reggio ». Alipomaliza masomo alipewa
upadirisho kwa mkono wa Kardinale Gennaro Portanova, tarehe 20/09/1902. Siku
ile alionyesha kwa watu wote nia yake ya kuwa mtumishi mwaminifu kwa Kristu;
aliwaamuru wazazi na marafiki wake wamuombee ili Moyo wa Yesu ipate kumuongoza
katika njia ya utakatifu. Ndipo akaagana ya kwamba atapiganisha zambi na atabaki
mbele ya uso wa Mungu siku zote za maisha yake.
Padri mkubwa wa parokya « Pentidattilo »
Muda wa myaka miwili alikuwa kiranja wa darasa la Seminario. Kisha kwa mwaka
1904, amechaguliwa kuwa padri mkubwa wa « Pentidattilo », mji ndogo wa «Aspromonte
», kwenyi kulikuwa umaskini, wengi hawakusoma, wengi walikuwa bila kujua mambo
ya dini, na kwenyi wakaaji walibaki katika ukimya hata kama walikuwa na magumu
nyingi. Bila kubakilia tu kwa mafundisho, Catanoso anakamilisha utumishi wake wa
uchungaji akijitolea kabisa kwa wote. Aliungana na wakaaji katika furaha na
magumu yao.
Tangu wakati huo, watu walitambua ndani mwake kipaji cha ubaba; na bila kukawia
watu walianza kumuita «Padre » yaani Baba. Watu walizidi kumuita kwa hiyo jina
siku zote. Kwa sababu alikuwa mtu mzuri na mwema kwa wote; hiyo ilitambulisha
kipaji yake ya Padri na mchungaji.
Katanoso alikuwa na juhudi katika utangazaji wa Neno la Mungu, katika mafundisho
ya Elimu ya kikristu, na katika ibada ya fumbo ya imani yetu, alijitolea kwa
Sakramenta ya Utubio, alisaidia jamaa zilizokuwa na magumu, alikuwa pia na
kipaji ya upekee kwa wagonjwa. Kwa ajili ya vijana wenyi hawakuweza kusoma,
Katanoso alianzisha masomo ya bila kulipa, na pale alikuwa pia mwalimu.
Padri Katanoso alisikilizana na aliungana na ma padri wakubwa wa Parokia jirani
katika utangazaji wa Neno la Mungu na katika ibada ya Sakramenta ya Utubio.
Missionario wa «Sura Takatifu »
Huko « Pentidattilo », Gaetano alikuwa na ibada kwa Sura ya Bwana wetu
Yesu Kristu aliyeteseka. Ndipo alikusudia kuendelesha ibada hiyo katika maisha
ya kiroho ya wakaaji wote. Na alialika ma padri na wakristu wote kwa utangazaji
wa Neno la Mungu ili watu wafikie hatua ya Kuongoka moyoni, wakipiganisha zambi
zote, hasa zambi ya kupuhuza na ya kuzarahu siku kuu zenyi Eklezia inasherea.
Ndipo akasema: «Sura Takatifu » ndiyo maisha yangu, yeye ni nguvu yangu;
na tena: «Yesu ana lazima ya wa Veronika wengi kwa kupiganisha zambi ya
upuhuzi na ya kuzarahu vitu vya dini; ana lazima pia ya Wakirene wengi kwa
sababu ya uzito wa msalaba; hasa misalaba ya wamaskini wenyi hawana nguvu na
hawapate watu wenyi wanawasaidia ».
Kwa furaha alilinganisha ibada kwa «Sura Takatifu » na ibada ya Ukaristia
Takatifu. Ni wazo hilo lenyi alitambulisha aliposema: «Ibada kwa Sura
Takatifu ina msinji wake kwa kitambaa ya Veronika, yenyi Bwana wetu Yesu Kristu
anatumia kwa kupanguza damu yake kuu kama alama Sura yake ya umungu. Hii ni
yenyi Eklezia ilibaki nayo na ni yenyi tunaabudu. Alakini kama tunapenda kuabudu
kweli Sura ya Yesu, isipokuwa tu Sura, hiyo sura inapatikana ndani ya Ukaristia
Takatifu; Mwili na Damu ya Yesu Kristu inapatikana ndani ya Hostia nyeupe, Sura
ya Bwana wetu. Na ginsi kristu ipo tena ndani ya kila mtu mwenyi kuteseka,
anajikaza kuleta sura ya Muumbaji kwa watu wenyi zambi».
Kwa mwaka 1918, Gaetano alikuwa « Misionario wa Sura Takatifu »,
akiwaandikia ma Padri wa « Turisi » katika Ufaransa. Mwaka ifwatayo
(1919) aliunda katika Parokia ya « Pentadattilo » « la Pia Unione del Volto
Santo » « yaani Muungano wa ibada kwa Sura Takatifu ». Kisha akaunda Jarida
mwenyi alionyesha mafaa ya hiyo ibada.
Mwenyi Kuanzisha «O.C.P. » (Opera dei Chierici Poveri) Yaani «Utumishi wa ma
Padri wa maskini »
Gaetano alitambua kama maendeleo ya wakaaji kwa ngambo ya Kiroho na Kimwili
haiwezekane bila utumishi wa uchungaji unaotimizwa na ma padri. Ndipo aliunda «
O.C.P. » yaani «l’Opera dei Chierici Poveri » akiwa na niya ya kuwatolea wa
vijana, zaidi wenyi hawajiweze, ile iliyo ya lazima kwa maisha na maadibisho yao
ili wapate kuwa ma Padri. Ndipo akaandika
« Tutiye pamoja nguvu yetu yote ili tupane kwa Eklezia ma Padri wengi na
watakatifu, tukisaidia uwito ya wa maskini. Ni kwa namna ya upekee ndani ya
vijiji vyetu kwenyi kunapatikana mauwa nzuri sana yenyi inachunga mkono yenyi
kuivuna na kuipanda katika shamba la Bwana. Hiyo inaonyesha kama siyo uwito ndio
inakosa, kama vile wanasema wamoja wenyi hawana niya ya kusaidiana »; na
akaongeza: «Ningelipenda damu yangu yote igeuke kuwa machozi ikawa kwa hiyo
majitoleo naweza kupeleka mbele uwito nyingi ya umaskini, yenyi itapunguza kesho
magumu ya Eklezia, Mama yetu, na magumu ya roho nyingi zinazopata nguvu kwa
ajili ya utumishi wa ma padri ».
Utumishi wa uchungaji pa « Reggio Calabria »
Tangu mwaka 1921 mpaka mwaka 1940, katika muji wa « Reggio », Gaetano
alikuwaka Padri mkubwa wa Parokia ya «Maria Mtakatifu wa Utakaso » (Santa
Maria della purificazione). Huko, aliposaidiwa na ndugu yake Padri Paskalino
(Pasqualino), aliendelesha kwa nguvu kazi yenyi alianzisha. Katika utumishi
wake, alipatia nafasi ya upekee kwa Ibada ya Ukaristia, Mahubiri, Katekismo,
Sakramenta ya Utubio, kuwatembelea watu, kuwasaidia maskini, wagonjwa na wenyi
wanazulumiwa; utumishi kwa ajili ya uwito ya wa vijana kwa kuwa ma padri,
kuwapokea wote wenyi walimkimbilia.
Hata kama wakubwa wake walimuongezea kazi zingine, mara nyingi nguvu kidogo,
hakuregea hata mara moja katika utumishi wake. Kazi waliomuongezea ni hizo
zifuatayo Mwongozi wa kiroho kwa Seminario (1922-1949), mwongozi wa kiroho
kwenyi Ospedali (19221933), mwongozi wa kiroho wa ma Bikira wapatikanao katika
muji; alishurulika na maungamo kwa wafungwa (1921-1950), alikuwa akishurulika na
mambo ya upekee ya kiroho kuhusu Sakramenta ya Utubio kwenyi Katedrale, yaani «
canonico penitenziere della Cattedrale » (1940- 1963), alikuwa mwongozi wa «
Pia Unione del Volto Santo », wakamutosha Pentidattilo na kumupeleka «
Reggio » kwa mwaka wa 1950 na dekreto ya arkiaskofu Demetrio Moscato
wa Salerno, aliyepewa na Papa wa Roma mamlaka ya kuongoza miji ya « Reggio»
na ya «Bova».
Muundaji wa jamaa la ma bikira wa «Veronika wa Sura Takatifu »
Katika myaka yenyi alipitisha huko Aspromonte, Catanoso alipata magumu yenyi
kuelekea maisha pamoja na watu na inayoelekea mambo ya dini. Kwa mwaka wa 1920
aliandika maneno yafuatayo: «Nilipotembelea vijiji vingi vya milima ya
Calabria, na nilipohubiri ndani ya parokia nyingi za Arkidioseze, nilisikia
huruma nyingi sana nilipoona watoto wengi wenyi kuteseka, vijana wengi wenyi
kukosa waongozi katika maisha yao, kanisa nyingi katika hali ya umaskini,
Tabernakoli nyingi zisizopambwa, ma padri wenyi kuteseka, na wenyi kukosa
wasaidiaji ». Ndipo akaanza kukamilisha wazo lake la kuanzisha jamaa moja la
ma Bikira wenyi kuwa na Ibada kwa Sura Takatifu ya Yesu na wenyi kuwa na
utumishi wa kusaidia ma Padri kwa kazi mbalimbali.
Kwa mwaka 1934, akishukuriwa na Mtakatifu « Luigi Orione », rafiki yake
wa tangu zamani, aliunda jamaa la «Ma Bikira Veronika wa Sura Takatifu ». Jamaa
hilo lilikubaliwa kwa mwaka 1953 na arkiaskofu «Giovanni Ferro » na kisha
likakubaliwa na Papa wa Roma.
Gaetano alisema kama ma bikira wanapashwa kuwa watu wenyi wanajua kuzungumuza na
wakaaji, wenyi kumpenda Bwana wetu Yesu Kristu wakiishi katika unyenyekevu,
wenyi hawateseke kama katika muji kwenyi walitumwa kuna nyumba na shamba. Ni
watu wasiokuwa na tamaa mbaya, watu wenyi kujitolea, wenyi kusaidia Eklezia.
Aliongeza pia yafuatayo: « Nafasi yako ni ile yenyi wengine wanazarahu, kati
ya watu wa maskini sana na wanyenyekevu ». Kufuatana na kanuni hizo
aliongoza jamaa hilo la ma bikira akilisaidia kwa kupiganisha magumu. Jamaa hilo
liliendelea ndani ya Parokia nyingi za Arkidioseze ya Reggio na zingine.
7. Hekalu moja la bwana
Kwa maendeleo ya ibada hiyo yenyi ilikuwa na nafasi ya lazima ndani ya maisha
yake ya kiroho na katika utumishi wake alianza kujengesha Hekalu akikubali
kuiweka kwa ulinzi wa Sura Takatifu. Lakini kifo ilipofika kwake hakuweza
kutimiliza hilo wazo lake la kujenga Hekalu. Lakini neema za Mungu zilimupatia
nyingi iliyo ya lazima. Gaetano Catanoso alijazwa na neema ya kufanya mwili wake
kuwa Hekalu ya kiroho ya Bwana (cf. 2 Wakorinto 6, 26). Hiyo ilitambulika
na wakaaji wa Reggio kufuatana na namna yake ya kuishi nao.
Watu wengi walimukimbilia na matumaini; hasa arkiaskofu wa muji, ma padri, ma
bikira (watawa wa kike), wanafunzi wa ku seminario, na wakristu wengine wengi.
Hawa wote aliwapokea vizuri na aliwaalika wote pamoja naye kwa kumshukuru Mungu,
kwa kupiganisha mabaya, kwa kutenda mema kila mara.
Pamoja na wa maskini kwa hela (kwa faida) ya wa maskini
Kama mutangazaji kamili wa Enjili, Catanoso hakutafuta kujitakatifuza yeye
mwenyewe; lakini yenyi alisema, yenyi aliandika, na kazi aliotimiza
zilitambulisha maisha yake ya uaminifu kwa Kristu. Pia, aliendelea kuhimiza watu
katika maisha yao ya kiroho. Alijitolea kwa kuendelesha hali ya dini huko
Calabria.
Gaetano Catanoso alipiganisha mabaya, magumu ya masikilizano iliyokuwa kati ya
wakaaji. Ukosefu wa masikilizano ilikuwa moja ya vinyume vya zambi. Ndipo, kwa
nguvu ya mapendo na ya unyenyekevu, alitafuta kuwarudishia wa maskini haki yao.
Katika muji alipiganisha yoyote yenyi haikuambatana na mapenzi ya Mungu.
Mafaa ya ukaristia na ya ibada kwa Maria Mtaka-Tifu
Gaetano aliheshimu maisha yake ya kiroho; na aliweza kuiambatanisha na matendo
yake ya mapendo na sala. Misa yenyi alihazimisha kila siku, na ibada ya kuabudu
Sakramenta takatifu ya altare zilikuwa moyo wa maisha yake ya upadri. Hiyo yote
ilimusaidia kwa utumishi wake wa utangazaji. Kitabu ya lazima aliyoandika na
yenyi inayoelekea kwa namna ya upekee mafaa ya Ukaristia Takatifu ni hii: «L’Ora
eucaristica sacerdotale », kitabu hiki kimeandikwa katika mwaka wa 1915.
Catanoso alijitolea sana, alijikatalia, na alipenda sana Sakramenta ya Utubio.
Bila kunungunika, alipokea na imani ndani ya maisha yake magonjwa na magumu hata
kwa siku za mwisho za maisha. Alipiganisha sana zambi na alikuwa na juhudi
kamili katika mahubiri, yaani katika utangazaji wa Enjili ya kuongoka moyoni.
Yeye mwenyewe , kwa mwaka wa 1929 alijitolea kama sadaka kwa Moyo wa Yesu
akitaka kuongeza ndani ya mwili wake yenyi inakosa mateso ya Kristu kwa faida ya
mwili wake iliyo Eklezia (cf. Wakolosi 1, 24). Gaetano alikuwa pia na
ibada kwa Bikira Maria; na aliwaalika ma bikira (yaani watawa wa kike) wa jamaa
lenyi aliunda yeye mwenyewe kwa ibada hiyo. Aliwaalika pia wakristu wote kwa
ibada hiyo kwa Bikira Maria. Tangu utoto wake, alikuwa mwenyi kupenda sala. Kila
siku hakukuwa anakosa kusali akitumia Rozario na aliendelea kusali na juhudi, na
moyo wa ibada mpaka siku yake ya kufa. Alama la Rozario lilikuwa kila mara
mikononi mwake.
Kifo
Hata katika uzee wake, kufuatana na ginsi iliwezekana, Gaetano hakuacha kutimiza
mapashwa yake ya upadri na utumishi wake wa utangazaji wa Neno la Mungu. Hiyo
yote ilizidi kumsaidia kujitayarisha vizuri kukutana na Mungu milele. Katika
magonjwa yake ya mwisho, mara nyingi alikuwa akisema kwa furaha kubwa: «
Ginsi Bwana alivyo mwema! Ginsi Bwana alivyo mwema!».
Akijazwa na nguvu za Sakramenta, Gaetano Catanoso alikufa katika bali ya utakaso
tarehe 4/04/1963 huko Reggio katika nyumbamama la jamaa la ma
bikira (yaani watawa wa kike) lenyi yeye mwenyewe alianzishaka.
Watawa na watu wengi, na kwa namna upekee wenyi walikuwa wakimuangalia kama
mtakatifu, walihazimisha ibada ya maziko kwa kumlaga padri Gaetano Catanoso.
Ibada hiyo ya maziko ilisomwa na Arkiaskofu aliyeshuhudia kama alimjua vizuri
Catanoso. Na hakuwa na masito ya kushuhudia ya kwamba «Catanoso alikuwa Padri
mwenyi ibada sana, na mwenyi alifundisha, katika maisha yake, ginsi ya kumpenda
na kumtumikia Bwana». Tarehe 04/05/1987, Papa Yoane Paulo wa pili
alimwongeza Padri Gaetano Catanoso kwa majina ya Wenyi Heri.
|